728x90 AdSpace

Wednesday, August 27, 2014

CAPITAL ONE CUP:MANCHESTER UNITED YATUPWA NJE NA MK DONS




Bundi ameendelea kutamba katika anga la klabu ya Manchester United baada ya hapo jana klabu hiyo yenye masikani yake katika dimba la Old Trafford kubamizwa goli 4-0 na klabu ya daraja la chini ya Mk Dons na hivyo kuiaga michuano hiyo kwa msimu huu.


Huu ni mchezo wa tatu wa mashindano kwa United kucheza ikiwa chini ya kocha mpya Mdachi Louis Van Gaal akiwa ameambulia sare moja tu na kupoteza michezo miwili ndani ya wiki moja na nusu.

Hii ni mara ya pili kwa Klabu ya Manchester United kutolewa katika mzunguko wa pili tangu ilipofanya hivyo mwaka 1995 pale ilipotupwa nje ya michuano hiyo na klabu nyingine ya daraja la chini ya York City.


Dons ilipata magoli yake kupitia wachezaji wa mkopo Will Grigg (kutoka Brentford) aliyefunga mara mbili huku kinda wa Arsenal aliyeko klabuni hapo kwa mkopo Benik Afobe naye akifunga mara mbili mbele ya mashabiki 26,969 huku mfumo wa 3-5-2 ukionekana dhahiri  kuwashinda walinzi wa Manchester United.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: CAPITAL ONE CUP:MANCHESTER UNITED YATUPWA NJE NA MK DONS Rating: 5 Reviewed By: Unknown