728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, August 18, 2014

    DEMBA BA-MOURINHO HAKUNIPANGA KWAKUWA SIKUWA STAA


    Habari na Paul Manjale
    Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Chelsea Msenegal Demba Ba amemtupia kombora kocha wake wa zamani katika klabu hiyo Mreno Jose Mourinho akimtuhumu kuwa hakumpa nafasi ya kuonyesha kipaji chake na badala yake alitoa nafasi kulingana na majina.

    Ba ambaye kwa sasa amehamia klabu ya Besiktas ya Uturuki alijiunga na klabu ya Chelsea  iliyokuwa chini ya Kocha Muhispania Rafael Benitez  akitokea Newcastle United januari 2013 kwa kitita cha paundi milioni 7 na kufunga magoli 14 katika michezo 23 aliyoanza kikosi cha kwanza.

    Ba akiongea na gazeti la The Sun amemlaumu kocha Jose Mourinho kuwa yeye ndiye aliyekuwa kikwazo cha yeye kufanya vizuri katika klabu hiyo kwa sababu alipendelea kuwatumia zaidi washambuliaji Samwel Eto’o na Fernand Torres badala yake kwasababu ya majina yao.

    Alisema “Kuna wakati unapokuwa kwenye klabu yenye nyota wengi ,majina hupewa kipaumbele zaidi kuliko takwimu.Kwa bahati mbaya ilikuwa hivyo kwa upande wangu.Nilipewa nafasi wakati  Eto’o na Torres hawakuwepo”alisema nyota huyo mwenye miaka 29.

    “Lakini nina furaha nilihama kutoka Newcastle na kutua Chelsea na nikapata nilichokipata.Nina marafiki wengi hapo.Eden Hazard ni rafiki yangu mkubwa,niko karibu na Ivanovic pia.Nawatakia kila jema ili waibuke na taji la ligi msimu huu.
     

    JE ILIKUWAJE AKASHINDWA KUTUA KWA MKOPO ARSENAL?
    Wakati huohuo pia Demba Ba alichua kuwa alikuwa karibu kutua Arsenalkwa mkopo  lakini uhamisho huo ulizimwa dakika za mwisho na kocha Jose Mourinho kwa kuwa hakutaka kutoa siraha kwa mpinzani wake.

    Ba “Uhamisho ulikuwa karibu nilibakisha kufanya vipimo vya afya lakini ilishindikana.Jose(Mourinho) hakutaka kuwapa mshambuliaji ambaye anaweza kufunga magoli hasa baada ya ujio wa Mesut Ozil.

    KUELEKEA MCHEZO WA KUSAKA TIKETI YA LIGI YA MABINGWA DHIDI YA ARSENAL BA AMESEMA!!
    Tumejiandaa vizuri dhidi ya Arsenal tunataka kushinda mechi zote mbili na hatimaye kupata nafasi ya kucheza katika hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa.Kikosi chetu bado ni kichanga kina vijana wengi wanaotaka kujifunza wanaoutaka mpira muda wote.Hatuna aina ya washambuliaji kama walioko Chelsea lakini tutahakikisha tunawashinda Arsenal kama walivyofanywa pale Stamform Bligde msimu uliopita kwa kichapo cha goli 6-0.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DEMBA BA-MOURINHO HAKUNIPANGA KWAKUWA SIKUWA STAA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top