728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 08, 2014

    SOUTHAMPTON NAYO BIZE KUSAJILI




    Klabu ya Southampton baada ya kutawala sana soko la usajili msimu huu kwa kuuza nyota wake mahiri sasa nayo imeanza kusajili ili kujipanga upya baada ya kuridhika na mauzo iliyoyafanya.

    Klabu hiyo inayotumia dimba la St Mary’s baada ya kumsajili mshambuliaji Grazziano Pelle,Ryan Betrand na Dusan Tadic  sasa imefanikiwa kumnasa kwa mkopo kiungo wa klabu ya Inter Milan Mualgeria Saphir Taider 22 ambayo aliiwakilisha vyema timu yake ya taifa katika michuano iliyoisha ya kombe la dunia.

    Katika usajili huo imeshuhudiwa pia klabu hiyo ikikubali kumtoakwa mkopo  mshambuliaji wake Pablo Osvaldo kwenda klabu ya Inter Milan huku kukiwa na makubaliano ya kufanyika mabadilishano rasmi mwisho wa msimu.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SOUTHAMPTON NAYO BIZE KUSAJILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top