728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 15, 2014

    TONY PULIS AACHIA NGAZI CRYSTAL PALACE



    Habari na Paul Manjale
    Pulis akishangilia moja kati ya mabao ya Crystal Palace

    Aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Crystal Palace Tony Pulis ( 56) ameachana na klabu hiyo zikiwa zimebaki saa 48 kabla  ligi ya Epl haijaanza kutimua vumbi jumamosi hii.Pulis alijiunga na klabu hiyo novemba 2013 akichukua nafasi ya kocha aliyetimuliwa Ian Holloway baada ya mwenendo mbaya katika ligi.

    Tony Pulis anaondoka baada ya msuguano wa mara kwa mara na uongozi wa klabu hiyo hasa mwenyekiti Steve Parish katika masuala mazima ya usajili yaliyopelekea kuwakosa nyota kama Gylfi Sigurdsson na Steven Caulke.Mpaka sasa Palace imeshawanasa nyota kama Chris Kettings na Brede Hangeland, Fraizer Campbell na Martin Kell.

    Pulis anakumbukwa kwa kuinusuru Palace kushuka daraja baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya klabu ya Chelsea na sare ya bao 3-3 dhidi ya klabu ya Liverpool kulikopelekea kocha huyo kutwaa tuzo ya LMAO (Kocha bora wa msimu akifungana na kocha wa klabu ya Liverpool Brendan Rodgers).Palace inabaki mikononi mwa kocha wa muda Keith Parish
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TONY PULIS AACHIA NGAZI CRYSTAL PALACE Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top