728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, August 07, 2014

    SPURS YAMNASA DEPAY





    KUTOKA THE MIRROR:Habari zinasema kwamba  vilabu vya Tottenham na Psv vimefikia makubaliano juu ya usajili wa winga mahiri wa Kidachi Memphis Depay.

    Katika makubaliano hayo ambayo awali ilidhaniwa kuwa Tottenham wangetoa kiasi cha  Euro milioni 20 ili kumnasa nyota huyo aliyetamba vilivyo akiwa na kikosi cha timu ya taifa ya Uholanzi (The Orange) katika fainali za kombe la dunia nchini Brazil.

    Katika makubaliano mapya klabu ya Tottenham imekubali kutoa kitita cha paundi milioni 10 pamoja na nyota wake wa Kibelgiji Nacer Chadli.Chadli aliyetua Tottenham msimu uliopita amejikuta akiwa nje ya mipango ya kocha mpya Muagrentina  Mauricio Pochettino.

    Depay anaondoka PSV licha cha kutakiwa kubaki japo kwa msimu mmoja katika ligi ya Eredivisie na aliyekuwa kocha wake wa timu ya taifa Louis Van Gaal.
    Depay akishangilia moja kati ya mabao aliyofunga
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SPURS YAMNASA DEPAY Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top