728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 05, 2014

    MASTAA WASHITUSHWA XAVI KUSTAAFU SOKA LA KIMATAIFA



    Baada ya kiungo wa klabu ya Barcelona Xavi Hernandez kutangaza kustaafu kuchezea timu ya taifa ya Hispania leo jumanne wachezaji mbalimbali duniani wameshitushwa na uamuzi huo.Baadhi ya wachezaji hao ni kiungo wa zamani wa klabu ya Arsenal Emanuel Frimpong,mlinda mlango wa klabu ya Liverpool Pepe Reina,kiungo wa Arsenal Santi Cazorla na mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Fernando Torres.

          Frimpong amesema “Dunia imepoteza kiungo bora zaidi wa kati kuwahi kutokea”

    Xavi mwenye umri wa miaka 34 alianza kuitumikia timu yake ya taifa maarufu kama La Furia Roja mwaka 2000.Mpaka anastaafu Xavi amefanikiwa kuichezea kokosi hicho  jumla ya michezo 133 katika  miaka 14 ya machozi,jasho na damu.

    Xavi anastaafu akiwa ameiwezesha Hispania kutwaa mataji makubwa matatu ambayo ni kombe la dunia (2010) na  mataji mawili ya Ulaya maarufu kama Euro (2008 na 2012) huku mwaka 2008 akichaguliwa kuwa mchezaji bora wa michuano hiyo.

    Xavi anastaafu baada ya kushindwa kuivusha La Roja kuingia japo hatua ya makundi katika fainali za dunia za mwaka huu zilizotimua vumbi nchini Brazil na timu ya taifa ya Ujerumani kuibuka mabingwa. 


















    @Paul Manjale
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MASTAA WASHITUSHWA XAVI KUSTAAFU SOKA LA KIMATAIFA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top