728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 19, 2014

    BILIC- ARSENAL ISITEGEMEE MTEREMKO USIKU WA LEO




    Kocha mkuu wa klabu ya Besktas ya Uturuki Mcroatia Slaven Bilic ameionya klabu ya Arsenal kuwa isitegemee kupata ushindi rahisi itakapokutana na vijana wake katika mchezo wa kusaka tiketi ya kucheza hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa Ulaya utakaopigwa leo jijini Instanbul katika dimba la Ataturk Olympic.
    Bilic akitoa maelekezo dimbani

    Bilic ambaye ni kocha wa zamani wa vilabu vya Westham United na Everton amesema “Hatuko hapa kupiga picha na wachezaji wa Arsenal uwanjani bali tuko hapa kupambana mpaka dakika ya mwisho.Usitegemee kuona wachezaji wetu wakipiga picha na Alexis Sanchez,Olivier Giroud ama Mikel Arteta or wakigombea jezi za Arsenal wakati wa mapumziko,tunaamini tunaweza kufuzu na tutafanya kila njia kuhakikisha hilo linafanikiwa.
    Slaven Bilic akivuta sigara baada ya mechi

    Tunawajua wapinzani wetu vizuri na wengi wanawapigia chapuo kufuzu lakini hii haituzuii kupambana na hatimaye kuwatupa nje ya michuano ya Ulaya.
    Itazame nembo ya ligi ya mabingwa nyuma yangu,wanasema picha inaongea maneno elfu.Itazame nembo hiyo,hapo ndipo tunapopataka,huo ndiyo mpango wetu na hiyo ndiyo ndoto yetu” Alimaliza Bilic
    Katika mchezo huo klabu ya Arsenal itamkosa mlinzi wake wa kushoto Kierran Gibbs na mshambuliaji Yaya Sanogo ambao wote ni majeruhi huku Laurent Koscienly akisafiri na timu licha ya kuwa majeruhi wa misuli.






    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BILIC- ARSENAL ISITEGEMEE MTEREMKO USIKU WA LEO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top