728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 10, 2014

    INGLESIA MARADONIANA (KANISA LA MARADONA)




    Kwa mujibu wa neno la kanisa hili,soka ni dini na kama ilivyo kwa dini yoyote ile kuwa na Mungu.Mungu wa soka ni Muargentina na jina lake ni Diego Armando MaradonaDini hii ilianzishwa tarehe 30 0ctober 1998 huko Rosario,Argentina na wafuasi wa  Maradona ambao wanaamini yeye ndiye mchezaji bora kabisa kuwahi kutokea .

    Mpaka leo dini hii ina wafuasi zaidi ya 100,000 katika nchi zaidi ya 55 duniani kote.Baadhi ya majina machache maarufu yaliyo na uhusiano wa moja kwa moja na kanisa/dini hiyo ni pamoja na Gary Lineker,Ronaldinho,Mauricio Pochettino(Kocha wa klabu ya Tottenham Hotspurs).

    Waasisi wa dini hii ni Hernan Amez,Alejandro na Hector Campomar ambapo hutumia autography/historia ya maisha ya Maradona badala ya Biblia

                                                   
    Mapri wa kanisa
    Muumini akisujudu
    Ndani ya kanisa



    AMRI KUMI ZA KANISA/DINI HIYO

    1.       Mpira usitiwe doa/alama/uchafu kama D10S alivyoagiza

    2.       Penda soka kuliko vitu vingine

    3.       Onyesha/tangaza mapenzi yako ya dhati katika mchezo wa soka

    4.       Zitetee rangi za Argentina

    5.       Yatangaze maneno ya Diego Maradona pande zote za dunia

    6.       Abudu kwenye hekalu alilohubiria/fundishia

    7.       Usilitaje bure jina la Diego Maradona katika jina la klabu moja

    8.       Shika mafundisho ya kanisa la Maradona

    9.       Fanya jina la Diego liwe jina lako la pili pamoja na la watoto wako

    10.   No ser cabeza de termo y que  no se te escape la Tortuga  (Usiwe mkaidi/kibuli na usiache hua/mdhaifu akutoroke)


           JE,D10S NI NINI?
                 Dios-Ni jina la Kihispania likimaanisha Mungu
                 10 -   Namba ya jezi ya Maradona

          SALA   Diego wetu uliye kiwanjani,mkono wako wa kushoto utukuzwe,



                    tuletee maajabu yako.Fanya magoli yako yakumbukwe duniani mpaka mbinguni,

                 tufanyie miujizayako  kila siku,



               wasamehe waingereza kama sisi tulivyowasamehe Mafia/Wahuni    wa Napoli,



               Usiache ukamatwe Offside na utuokoe kutoka kwa Joao Havelange na Pele.Diego

       SIKUKUU:June 22 (Tarehe hii huwa ni sikukuu  ya Pasaka kwa wafuasi wa dini ya Maradoniana kuadhimisha /kukumbuka mechi kati ya Argentina na England ambayo Diego Maradona aliiongoza..

    Argentina kutwaa ubingwa wa dunia mwaka 1986
    .
    Katika sikukuu hiyo Hernan Amez,Alejandro na Hector Campomar huvaa majoho/kanzu meupe huku wakiwa wameshikilia mpira na taji la miba miba.

    October 30 ni kimbukumbu ya kuzaliwa kwa maradona ambapo kila ifikapo tarehe hii huadhimishwa sikukuu kubwa ikiambatana na Misa,Ubatizo,Harusi na shamra shamra mbali mbali.................itaendelea









    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: INGLESIA MARADONIANA (KANISA LA MARADONA) Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top