728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, August 27, 2014

    MOYO WAMSTAAFISHA SOKA MLINDA MLANGO WA ARSENAL




    Mlinda mlango wa zamani wa klabu ya Arsenal Muhispania Manuel Almunia (37) amelazimika kustaafu soka baada ya kubainika kuwa ana matatizo katika moyo wake.




    Almunia ambaye aliichezea klabu ya Arsenal kwa misimu minane kabla ya kutua katika klabu ya Watford misimu miwili iliyopita amebainika kuwa na tatizo hilo baada ya kushindwa mara tatu kufuzu vipimo vya afya katika klabu ya Cagliari iliyokuwa tayari kumsajili katika dirisha hili usajili barani Ulaya.


    Almunia ambaye pia ni mlinda mlango wa zamani wa klabu ya Celta De Vigo ya Hispania anatundika gloves zake baada ya miaka ishirini ya kucheza soka la kulipwa katika nchi za Hispania na England huku mafanikio yake pekee yakiwa ni kucheza mchezo wa fainali wa ligi ya mabingwa wa Ulaya kati ya Barcelona na Arsenal mwaka 2006 ambapo Arsenal ililala kwa goli 2-1.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MOYO WAMSTAAFISHA SOKA MLINDA MLANGO WA ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top