728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 19, 2014

    ROJO ANUKIA MANCHESTER UNITED




    Baada ya habari mbaya za kipigo na kosa kosa za hapa na pale katika usajili hatimaye nyuso za furaha zimeanza kuonekana katika klabu ya Manchester United baada ya mlinzi Marcos Rojo (24) kutegemewa kusaini leo kujiunga na mabingwa hao wa zamani wa ligi ya Epl.

    Marcos Rojo ambaye ni mlinzi wa kushoto wa kutumainiwa wa klabu ya Sporting Lisbon ya Ureno na timu ya taifa ya Argentina anatarajiwa kuwasili leo makao makuu ya klabu ya Manchester United tayari kwa vipimo vya afya na kusaini mkataba wa miaka mine wenye kipengele cha kuongeza mmoja zaidi.Inaaminika Manchester United italazimika kutoa kitita cha paundi milioni 16 pamoja na winga wake mahiri wa Kireno Louis Nani kwa mkopo wa msimu mmoja.

    Louis Nani anatazamiwa kutua jijini Lisbon leo jumanne au kesho jumatano kufanyiwa vipimo vya afya kabla ya kumwaga wino kwa mara nyingine tena kuichezea klabu yake hiyo ya zamani kwa mkopo wenye kipengere cha kuwa wa kudumu baada ya msimu huu wa 2014-2015.

    Rojo ambaye wiki moja iliyopita aliingia matatani na kutishiwa kuadhibiwa na klabu yake baada ya kugomea mchezo wa kirafiki pamoja na mazoezi akishinikiza kuondoka klabuni hapo na kutua Manchester United kutimiza ndoto yake ya tangu utotoni.

    Usajili wa Rojo United unakuja wakati muafaka kwani klabu hiyo kwa muda wa mwezi mmoja itazikosa huduma za mlinzi wake aliyemajeruhi Luke Shaw hali iliyopelekea klabu hiyo kumtumia kinda Blackett katika mchezo wa ufunguzi wa ligi na kuambulia kipigo toka kwa klabu ya Swansea City ya Wales.

    Rojo pia ni tiba nyingine katika mfumo mpya wa 3-5-2 wa kocha Louis Van Gaal kwani licha ya kuwa mahiri sehemu ya ulinzi wa kushoto pia Muargentina huyo ni hodari achezapo kama mlinzi wa kati.

    JE,NANI ANAHUSIKA KUMSHAWISHI ROJO ATUE UNITED?
    Rojo akifanya mahojiano na kituo cha redio cha nyumbani kwao kiitwacho Continental mapema jana alisema “Nimevutiwa na Manchester United tangu kitambo sana nakumbuka Juan Sebastian Veron nikicheza nae katika klabu ya Estudiantes aliniambia mengi sana kuhusu klabu hiyo”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: ROJO ANUKIA MANCHESTER UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top