728x90 AdSpace

Wednesday, August 20, 2014

RAMSEY:SAMAHANI KWA KADI NYEKUNDU DHIDI YA BESIKTAS



Habari na Paul Manjale

Kiungo wa klabu ya Arsenal Aaron Ramsey amewaomba radhi mashabiki wa klabu hiyo baada ya kupata kadi nyekundu  juzi katika mchezo wa kusaka tiketi ya kufuzu kuingia hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa Ulaya.
Ramsey akiwa na moja kati ya tuzo zake alizonyakuwa msimu uliopita baada ya kuibuka mchezaji bora wa mwezi


Ramsey amesema “Asanteni mashabiki wote mliosafiri mpaka Uturuki kuja kutuunga mkono lakini samahani sana kwa kadi nyekundu niliyoipata katika mchezo huo.Natumaini wenzangu watashinda mchezo wa marudiano”.
Ramsey akitoka nje baada ya kupewa kadi nyekundu


Ramsey alitolewa uwanjani dakika ya 80 ya mchezo baada ya kuonyeshwa kadi ya pili ya njano kwa kosa la kumdondosha chini kwa kumvuta jezi nyota wa klabu ya Besiktas na kinda wa zamani wa klabu ya Arsenal Ozyikup.

Ramsey atalazimika kuwa mtazamaji katika mchezo wa marudiano utakaopigwa katika uwanja wa nyumbani wa klabu yake ya Arsenal wa Emirates jijini London wiki ijayo ambapo mshindi wa mchezo huo atakata tiketi ya kuingia katika droo ya hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa wa Ulaya.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: RAMSEY:SAMAHANI KWA KADI NYEKUNDU DHIDI YA BESIKTAS Rating: 5 Reviewed By: Unknown