728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 03, 2014

    JUMATATU NI KIVUMBI NA JASHO KATIKA FAINALI YA INTERNATIONAL CHAMPIONS CUP




    Safari hii ile derby ya North-East ya mahasimu wakubwa wa ligi ya Epl kati ya Manchesterb United na Liverpool inaanzia Marekani.Hii ni baada ya vilabu hivi wiwili kushinda michezo yao ya jana usiku katika kinyang’anyiro cha kombe la International Champions Cup.


    Manchester United jana usiku iliwabomoa mabingwa wa Ulaya klabu ya Real Madrid kwa jumla ya magoli 3-1 katika mchezo mkali uliokuwa na vuta ni kuvute katika vipindi vyote viwili huku vijana wa Luis Van Gaal wakionekana kuumudu vilivyo mfumo mpya wa 3-5-2.Katika mchezo huo magoli ya Manchester United yalifungwa na Ashley Young aliyefunga mara mbili na Javier Hernandez “Chicharito” alifunga mara moja huku lile la kufutia machozi la Real Madrid likifungwa na winga Gareth Bale kwa mkwaju wa penati.


    Liverpool nao hawakuwa nyuma kwani waliikimbiza watakavyo klabu iliyobaki jina ya Ac Milan na kuishindilia jumla ya magoli 2-0 katika mchezo uliofanyika katika dimba la Bank of America.Liverpool waliotumia mfumo wa 4-3-3 walionekana kuizidi ujanja klabu ya Ac Milan tangu mwanzo wa mchezo huo mpaka mwisho huku nyota wa mchezo huo akiwa ni kinda wa klabu hiyo  Jordan Ibe.


    Magoli yalifungwa na Joe Allen (16) na Suso (89)……………………Mchezo wa fainali kati ya Liverpool na Manchester United utafanyika jumatatu jijini Miami……….Je nani ataibuka mshindi?ni jambo la kusubiri na kuona…….
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: JUMATATU NI KIVUMBI NA JASHO KATIKA FAINALI YA INTERNATIONAL CHAMPIONS CUP Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top