728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 26, 2014

    PIGO ARSENAL!!HUENDA GIROUD AKAWA NJE KWA MIEZI MITATU




    Ndoto za kocha mkuu wa klabu ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger kutotaka kusikia habari za kusajili mshambuliaji mpya zimeingia mdudu baada ya mshambuliaji wake tegemeo Mfaransa Olivier Giroud kuhofiwa kuwa nje kwa kipindi cha miezi mitatu baada ya kuumia kifundo cha mguu jumamosi iliyopita.


    Giroud aliumia wakati akijaribu kuzuia mpira uliopigwa na mlinzi wa Everton Sylvian Distin zikiwa ni dakika chache tu tangu mshambuliaji huyo afungu goli za kusawazisha akitokea benchi kuchukua nafasi ya Mchile Alexis Sanchez ambaye alianza kama mshambuliaji wa kati.

    Habari kutoka ndani ya klabu ya Arsenal zinasema Giroud huenda akawa nje kwa kipindi cha karibu miezi mitatu baada ya jeraha lake kuonekana kubwa kuliko ilivyodhaniwa hapo mwanzo.Taarifa kamili za mwisho  juu ya lini hasa nyota huyo atakuwa nje ya dimba zitatolewa leo na madaktari bingwa wa klabu hiyo kwa kuaqnzia nyota huyo atakosa mchezo wa jumatano wa kusaka tiketi ya ligi ya mabingwa dhidi ya Besktas ya Uturuki.

    Kutokana na kadhia hiyo kocha Arsene Wenger atalazimika kuingia tena sokoni kusaka mshambuliaji mpya baada ya hapo mwanzo kutokuwa na mpango huo  huku kukiwa na habari ya kuwa karibu kumuuza mshambuliaji wake Mjerumani Lukas Podolski kwenda vilabu vya Juventus ama Wolsburg.
    Kati ya majina yanayotajwa tajwa kutua Emirates kuziba pengo la mshambuliaji Olivier Giroud ni pamoja na nyota wa klabu ya Manchester United Danny Welbeck,Loic Remmy na nyota wa Torino Alessio Cerci.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: PIGO ARSENAL!!HUENDA GIROUD AKAWA NJE KWA MIEZI MITATU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top