728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, August 20, 2014

    SUAREZ:NIMEKOMA SITONG’ATA TENA WAPINZANI

    Habari na Paul Manjale


    Mshambuliaji mpya wa klabu ya Barcelona Mruguayi Louis Suares (27) ameapa kuwa hatokuja kumng’ata mpinzani wake na kukiri kuwa amekuwa akipata msaada wa ushauri toka kwa mwanasaikolojia tangu alipozamisha meno yake kwenye bega la mlinzi wa Italia Georgio Chiellini wakati wa fainali zilizoisha za kombe la dunia nchini Brazil.
    Suarez akikagua meno yake baada ya kumng'ata Chiellini


    Suarez ambaye hivi karibuni alipunguziwa adhabu na mahakama ya michezo CAS na kuruhusiwa kufanya mazoezi pamoja na kucheza mechi za kirafiki amesema

     “Nawaambia mashabiki msiwe na shaka kwasababu sitorudia tena kitendo kile.Nimeongea na mwanasaikolojia wangu na ameniambia dawa ni kukubali kilichotokea  na kuomba radhi.Tayari nimeomba radhi na akili yangu kwasasa ni kuitumikia klabu yangu ya Barcelona.


    Wakati huohuo Suarez ameelezea furaha yake baada ya kucheza mechi yake ya kwanza akiwa na klabu ya Barcelona katika ushindi walioupata wa goli 6-0 dhidi ya klabu bingwa ya Mexico Club Leon.Amesema

     Siyo kuwa kucheza tu bali pia kuwa chumba kimoja cha kudalishia nguo na wachezaji kama Leonel Messi na Neymar kunanifanya nijisikie furaha sana”Inakufanya ujisikie furaha na hamasa kucheza npamoja nao.Sijioni kuwa nyota,nyota ziko angani.

    Niko tayari kucheza popote pale katika ushambuliaji.Nimecheza mechi nyingi nikitokea winga ya kushoto au winga ya kulia nikiwa na Liverpool kwa sababu Daniel Sturridge alikuwa akicheza namba 9.Hivyo sina tatizo kucheza nafasi yoyote ya ushambuliaji atakayonipanga kocha.

    Je,ni kweli aliikataa ofa ya


    Real Madrid?
    Suarez “Ndoto ya kuchezea Barcelona inaanzia miaka mingi sana,tangu nikiwa motto.Kila mtu anajua kwamba baadhi ya jamaa wa familia yangu wanaishi hapa.Kulikuwa na ofa toka vilabu vingi lakini ilipokuja Barcelona sikujiuliwa mara mbili ilikuwa ni kutimia tu ndoto”.

    “Nimekuwa nikipenda sana kuja Camp Nou nilikuwa hapa wakati Barcelona ikiifunga Madrid goli 5-0,Arsenal 4-1 na Espanyol 1-0 goli la Andres Iniesta”Alimaliza Suarez
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: SUAREZ:NIMEKOMA SITONG’ATA TENA WAPINZANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top