728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, August 07, 2014

    JE WAJUA YAKWAMBA NEWCASTLE ILIKATAA KUMSAJILI AARON RAMSEY?




    Moja kati ya maamuzi ambayo bado yanaitesa vilivyo klabu ta Newcastle United ni hatua yake ya kukataa kutoa dau kiduchu na kumpata kiungo Aaron Ramsey.

    Habari iko hivi…..Neil Bartholomew (msaka vipaji wa klabu hiyo) aliipasha habari klabu ya Newcastle juu ya kiungo mwenye kipaji kikubwa cha soka nchini Wales akiwa na klabu ya Cardiff .Baada ya taarifa hizo klabu ya Newcaster ilimtumia tiketi ya ndege Aaron Ramsey pamoja na wazazi wake kwa ajili ya kuja kufanya majaribio klabuni hapo.

    Baada ya majaribio ya mara kwa mara Newcastle wakaonekana kuvutiwa na mchezaji huyo kinda aliyekuwa na miaka 15 tu lakini kama ujuavyo usajili wa makinda kwa vilabu vingi huwa ni kama kucheza kamari tofauti na mchezaji mkubwa Newcastle wakakataa kutoa kiasi cha paundi 500,000 tu kumnasa Ramsey licha ya kuwa alikuwa na usongo sana wa kuichezea klabu hiyo.

    Kama ujuavyo ya Mungu mengi,baada ya miaka miwili ya juhudi na kujituma kwingi klabu ya Arsenal ilikuja na ofa nono kipindi kile ya paundi milioni 5 na kumnasa kinda huyo ambaye leo ni staa kweli kweli katika dimba la Emirates.
    Ramsey akiwa na moj kati ya tuzo za mchezaji bora wa mwezi

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: JE WAJUA YAKWAMBA NEWCASTLE ILIKATAA KUMSAJILI AARON RAMSEY? Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top