728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, August 14, 2014

    DORTMUND YAIFUNGA BAYERN NA KUTWAA SUPER CUP KWA MARA YA PILI



    Klabu ya Borussia Dortmund imeibamiza klabu ya Bayern Munich goli  2-0 na kutwaa taji la Super Cup kwa mara ya pili mfululizo kama ishara ya ufunguzi wa msimu mpya wa ligi ya Bundesliga.Borussia Dortumund ikicheza mbele ya mashabiki wake katika dimba lake la Signal Park Iduna mjini Frankfurt ilijipatia magoli yake kupitia washambuliaji wake Henrikh Mkhitaryan  aliyefunga goli la kwanza dakika ya 23 na Pierre-Emerick Aubameyang aliyefunga goli la pili dakika ya 62.
    wachezaji wa dortmund wakisherekea kikombe cha super cup

    Aubameyang na Grotzesk wakishangilia ushindi

    wachezaji wa dortmund wakishangilia goli la kwanza



    Huu ni ubingwa wa pili mfululizo wa Super Cup kwa klabu ya Borussia Dortmund baada ya kufanya hivyo mwaka jana kwa kuwafunga tena Bayern Munich kwa jumla ya magoli 4-2.Kivutio katika mchezo huu alikuwa ni mshambuliaji Pierre-Emerick Aubameyang ambaye baada ya kufunga goli alivaa kinyago cha Spider Man alichokuwa amekificha katika soksi zake muda wote wa mchezo.

    Katika mchezo huo Dortmund ilikuwa bila ya nyota wake Matt Hummels,Marco Reus na Ilkay Gundogan wanaouguza majeraha wakati Bayern ilikuwa bila ya nyota kama Frank Ribery aliye majeruhi,Arjen Robben na Basten Schwanstiger walio mapumzikoni.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DORTMUND YAIFUNGA BAYERN NA KUTWAA SUPER CUP KWA MARA YA PILI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top