728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 05, 2014

    RODWELL ATUA SUNDERLAND



    Klabu ya Sunderland imefanikiwa kumsajili kiungo wa klabu ya Manchester City Muingereza Jack Rodwell kwa mkataba wa miak mitano kwa ada ambayo haikutajwa.

    Rodwell anahama Manchester City ikiwa ni miaka miwili pekee tangu atue klabuni hapo akitokea klabu ya Everton kwa ada ya paundi milioni 12.


    Rodwell amefanikiwa kuichezea klabu hiyo jumla ya michezo 16 huku akiifungia magoli 2 yote yakiwa katika mchezo ambao Manchester City ilifungwa goli 3-2 dhidi ya klabu ya Norwich City katika msimu wa 2012-2013.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: RODWELL ATUA SUNDERLAND Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top