728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, August 03, 2014

    MAN CITY YAMTAKA LAMPARD KWA MKOPO

                                        


    Klabu ya Manchester City iko katika mawindo ya kumsajili kwa mkopo wa miezi sita(6) kiungo wa zamani wa klabu ya Chelsea Muingereza Frank Lampard (36).Lampard ambaye hivi karibuni alikamilisha usajili katika klabu ya New York City inayoshiriki ligi ya MLS akiwa kama mchezaji huru baada ya kunyimwa mkataba mpya na klabu ya Chelsea ameonyesha kumvutia kocha wa City Manuel Pellegrini. 


    Pellegrini anaamini Lampard atakuwa na mchango mkubwa sana hasa sehemu ya kiungo ya klabu hiyo ambayo imekuwa ikimtegemea zaidi kiungo Muivory Coast Yaya Tourekatika  kujenga mashambulizi na nyakati nyingine kuzuia timu inapokuwa matatani.

    Klabu ya New York City itaanza kukipiga MLS mwezi Machi mwakani hivyo Manchester City inataka kutumia mwanya huo ili kumtumia Lampard katika mechi za ligi kuu ya Epl pamoja na ligi ya mabingwa barani Ulaya maarufu kama Champions League.
    Wakati huohuo kocha Manuel Pellegrini amesema kuwa klabu yake haitofanya usajili mwingine zaidi mara itakapokuwa imemnasa mlinzi mahiri wa klabu ya Porto Mfaransa Eliaquim Mangala.




    @Paul Manjale






























    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MAN CITY YAMTAKA LAMPARD KWA MKOPO Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top