728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, August 18, 2014

    MOURINHO AJA NA DAWA YA KUZIFUNGA TIMU ZINAZOPAKI BASI



    Habari na Paul Manjale

    Kocha mwenye maneno mengi ya karaha Mreno Jose Mourinho amekitaka kikosi chake kujifunza kuzifunga timu zinazocheza mchezo wa kuzuia zaidi maarufu kama kupaki basi ili yasijekuwakuta ya msimu uliopita hata kufikia hatua ya kuukosa ubingwa wa ligi kuu.


    Mourinho amekiri kwamba kikosi chake kiliteleza msimu uliopita kutokana na kutokuwa na mbinu za kutosha kuzifunga timu zilizoingia uwanjani kupaki basi alitolea mfano mchezo dhidi ya West ham ulioisha kwa sare na kusema timu hiyo ilicheza soka la karne ya kumi na tisa (19).

    Mourinho anaamini nyota wake wapya Cesc Fabregas na Diego Costa watatatua tatizo hilo wakianzia na mchezo dhidi ya Burney usiku wa leo.

    Mourinho amekiri kuwa kikosi chake kimefanya mazoezi mengi katika kipindi cha maandalizi ya msimu (pre-season) kujaribu kuzifunga timu zinazochezesha wachezaji kumi nyuma ya mpira(kupaki basi).

    Mourinho amesema “Tunahitaji ubora katika mchezo wetu ,unapokuwa na mchezo wenye nafasi na muda ni rahisi kucheza mpira lakini unapokuwa huna nafasi na muda ,unahitaji ubora zaidi na umahiri katika umaliziaji.Tunalifanyia kazi hilo ili kuzizidi ujanja timu zinazoziba njia ya kuelekea golini.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: MOURINHO AJA NA DAWA YA KUZIFUNGA TIMU ZINAZOPAKI BASI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top