728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, August 22, 2014

    WENGER:RAMSEY ANA MENGI YA KUTUPA KULIKO FABREGAS



    Kocha mkuu wa klabu ya Arsenal Mfaransa Arsene Wenger anaamini kuwa anaweza kupata vitu vingi kutoka kwa kiungo wake Aaron Ramsey kuliko alivyovipata kwa kiungo wake wa zamani ambaye kwa sasa yuko katika klabu ya Chelsea Mhispania Cesc Fabregas.






    Wenger hakuweza kukwepa mkutano na waandishi wa habari bila ya kuulizwa alijisikiaje baada ya kumuona kiungo  wake wa zamani {Fabregas} akiwa amevaa jezi ya klabu ya Chelsea ambao ni wapinzani wao toka jiji la London. 


    Kocha huyo alijibu Jambo jema katika maisha ni kwamba mtu anapoondoka mwingine anakuja na kupiga hatua.Rasmey ana aina tofauti ya kiuchezaji ukimlinganisha na Fabregas ,lakini amepiga hatua na kuwa mchezaji mmoja kati ya wachezaji nyota.Kuna mengi yanakuja toka kwake.Bado ni mdogo ukimlinganisha na Fabregas na kuna matarajio ya kupata mengi zaidi toka kwake.”


    Pia Wenger anaamini kuwa Ramsey atakuwa klabuni hapo kwa muda mrefu zaidi na hivyo kuwa sehemu na kiungo cha mafanikio kuliko ilivyokuwa kwa Fabregas ambaye aliondoka klabuni hapo katika wakati ambao klabu ilihitaji zaidi huduma yake.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WENGER:RAMSEY ANA MENGI YA KUTUPA KULIKO FABREGAS Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top