728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, August 26, 2014

    KOCHA ATLETICO MADRID AFUNGIWA MECHI NANE NJE YA DIMBA




    Kocha mkuu wa klabu ya Atletico Mdrid Muargentina Diego Simeone amefungiwa jumla ya michezo minane na chama cha soka cha Hispania (RFEF) baada ya kutolewa nje katika mchezo wa pili wa kombe la Spanish Super Cup ijumaa iliyopita dhidi ya wapinzani wao wa jadi klabu ya Real Madrid.


    Simeone alitolewa nje ya eneo la kufundishia na mwamuzi David Fernandez Barbolan baada ya kulalamika mwamuzi wa akiba alikuwa akichukua muda mrefu mno kumruhusu mlinzi wake Juanfran kurejea uwanjani baada ya kufanyiwa matibabu yaliyotokana na kuumizwa na mchezaji wa Real Madrid.

    Kufuatia kitendo hicho kocha Simeone alimgonga kwa mkono kisogoni mwamuzi wa akiba Antonio Santos Pargana wakati akiondoka eneo la kazi la mwamuzi huyo.Pia kocha huyo mwenye vituko alipiga makofi ambayo yanaaminika kuwa ni ya kejeri  kwa mwamuzi huyo.

    Simeone atakosa michezo miwili kwa kosa la kulalamika,michezo minne kwa kumpiga mwamuzi wa akiba,mmoja kwa kupiga makofi ya kejeri na mwingine dhidi kwa kosa la kutazama mechi kipindi cha pili akiwa jukwaani.Kocha huyo pia amepigwa faini ya Euro 4,805 huku pia Atletico ikiamliwa kutoa cha Euro 2,800.

    RFEF pia imeshindwa kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya Mreno Cristiano Ronaldo ambaye picha za televisheni zilimuonyesha  akimpiga mlinzi wa Atletico Diego Godin dakika za mwisho za mchezo huo.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOCHA ATLETICO MADRID AFUNGIWA MECHI NANE NJE YA DIMBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top