728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 09, 2014

    0SCAR:NACHUKIA NIKIPOTEZA PASI




    Kiungo mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Mbrazil Oscar Dos Santoa (22) ameelezea kitu kinachomnyima usingizi na kumkera klabuni hapo.Akifanya mahojiano na jarida la klabu hiyo Oscar amesema…


    “Huwa nachukia sana pasi yangu isipomfikia mchezaji mwenzangu wa Chelsea.Mimi ni mtu mshindani sana na ninapenda kushinda kila mchezo.Nataka pasi zangu zote ziwafikie walengwa na mara zote napenda kufunga,ndiyo nilivyo”.


    “Kama mechi ni ngumu sitoki naendelea kupambana mpaka kieleweke.Mimi ni mchezaji mbunifu,mpambanaji napenda kutimiza majukumu yangu uwanjani.Napenda kutengeneza nafasi na pia kuwa na mpira mguuni.Nisipokuwa na mpira nafanya kila jitihada ili niupate na kuhakikisha napambana ili kuisaidia timu yangu iibuke na ushindi”

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: 0SCAR:NACHUKIA NIKIPOTEZA PASI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top