728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 08, 2014

    OKWI MASHABIKI NDIVYO TULIVYO...........


    MAKALA YA LEO
    Paul Manjale
     
    Moja kati ya sifa kubwa za mashabiki wa mchezo wa soka duniani ni kubadilika badilika kama vinyonga. Mashabiki wa soka ndivyo tulivyo  hatutabiriki kama ajari za barabarani,mchezaji tunayempenda sana ndiye tunayemchukia sana siku tu akifungasha vilivyovyake na kutimka. 

     Kilichomkuta Okwi jana uwanja wa taifa ni muendelezo tu wa kile ambacho kimekuwa kikiwakuta nyota wengi wa soka duniani kote.Kuzomewa kila dakika wawapo uwanjani.Samir Nasri,Robin Van Persie na Emanuel Adebayor ni baadhi tu ya wachezaji wanaokumbana na kadhia  hiyo karibu kila siku iendayo kwa Mungu.
    Okwi akifanya vitu vyake uwanjani juzi dhidi ya Gor Mahia
     Okwi anaingia katika orodha hiyo ya wachezaji wanaozomewa viwanjani kwasababu tu wametoka upande huu na kuhamia upande ule wa mji tena kwa watani wa jadi.Yanga kwenda Simba tena katika usajili wenye utata mkubwa. Swali la kujiuliza hapa ni kwanini Okwi alizomewa jana kiasi kile na mashabiki wanaodhaniwa kuwa ni wa klabu ya Yanga?Jibu liko wazi kabisa ni kwasababu ameiacha Yanga ikiwa mikono mitupu haina taji haina chochote na yeye kutimkia Simba. 

     Mashabiki wanamuona Okwi kuwa ni mkosefu na msaliti  mkubwa bila hata ya kutaka kujua nani anaongea ukweli kati yake na viongozi wa klabu yao.Hakuna tena shabiki wa Yanga anayemuongea Okwi kwa mazuri hata wale wachache walibahatika kuwa na namba zake za simu siyo ajabu nao wakawa wameshazifuta mpaka sana.Wanamchukia na kumlani kama mbu wa dengue.

     Mashabiki tunasau kuwa soka ni ajira kama zilivyo ajira nyingine hivyo mchezaji anapohama hapa na kwenda kule ama kule na kuja huku huwa ni katika kutafuta maslahi mazuri pamoja na mazingira bora kwa ajili ya soka yake.Ridhiki ya mtu iko miguuni kwake.

     Kama tujuavyo ili mchezaji yoyote yule aweze kucheza katika kiwango bora anahitaji mazingira yatakayompa nafasi ya kufanya hivyo kitu ambacho Emanuel Okwi anaamini kinapatikana Simba pekee na siyo kwingineko.

     Tumemuona jinsi Okwi wa Yanga alivyokuwa mpole kiwanjani kama faru wa kuchora, hakuwa na makeke wala vurugu zile tulizozizoea kuziona toka kwake.Hakuwa yule Okwi wa miaka miwili nyuma yule aliyechukiwa na karibu kila shabiki wa timu pinzani.

    Yule Okwi aliyefanya makocha wengi wafanye kazi ya ziada kuwafunda walinzi wao ili Mganda huyo asilete balaa. Swali la kujiuliza hapa ni kwanini nyota kama Thierry Henry ana Christian Ronaldo wanaabudiwa sana Arsenal na Manchester United licha ya kuwa walivikacha vilabu hivyo kitambo?Jibu ni kwasababu waliifanya kazi yao barabara,wakashusha mvua ya mataji pale Emirates na Old Trafford na kisha wakaondoka zao.

     Okwi ameondoka na deni Yanga,hakuondoka kama alivyoondoka Henry kwenda Barcelona ama Ronaldo kwenda Real Madrid.Je,zomea zomea ndiyo dawa ya kupoza maumivu ya kukimbiwa?sijui tuwaulize hao waliokwenda taifa jana kumzomea.....Okwi mashabiki ndivyo tulivyo!!
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: OKWI MASHABIKI NDIVYO TULIVYO........... Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top