728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, September 16, 2014

    CASCARINO:COSTA NI ZAIDI YA DROGBA



    Nyota wa zamani wa klabu ya Chelsea Muireland Tony Cascarino anaamini kuwa mshambuliaji mpya wa klabu hiyo Muhispania Diego Costa atakuwa bora zaidi ya gwiji na mchezaji mwenzie  raia wa Ivory Coast Didier Costa “Tito” alyeifungia klabu hiyo jumla ya magoli 157 katika misimu minane akitokea klabu ya Marseille ya Ufaransa.

    Cascarino akiwa na Denis Wise enzi akichezea klabu ya Chelsea


    Baada ya kumshuhudia Diego Costa akifunga magoli saba katika michezo minne ya Epl,Cascarino anaamini Costa ni bora hata zaidi ya yule Drogba  wa misimu kadhaa iliyopita.


    Cascarino amesema “Nafikiri Costa ni bora kuliko Drogba.Amekuwa akihaha kwenye eneo la adui muda wote bila kuchoka.Najua ni mapema,lakini nafikiri kuna njaa na hasira ndani yake na kwa kiasi fulani namuona yuko vizuri kinguvu kuliko Drogba.Lakini anapaswa kupunguza kidogo hilo na kuendelea na  njaa ile ile.Kama anaweza kufanya hilo na kuwa mbali na majeruhi hakuna shaka ndiye atakayeibuka kuwa mfungaji bora wa Epl msimu huu.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CASCARINO:COSTA NI ZAIDI YA DROGBA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top