728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, September 15, 2014

    KOPO LA CHUMVI CHAFU JIKONI CHAKULA KITAMU TAYARI MEZANI



                                                                   MAKALA YA LEO
     Allen Kaijage

     0655106767
     kaijagejr@gmail.com



     Thamani ya mtu ipo kwenye umuhimu wa mtu pia upendo kwa kitu au mtu upo kwenye thamani ya mtu au kitu husika.Sentesi hii si sheria ingawa imeegemea kwenye  ukweli .Ukitaka kujua ukweli wake angalia watu wanaoheshimiwa kwenye jamii wana umuhimu gani kwenye hiyo  jamii?,pia chunguza vitu vinavyopendwa na kuheshimiwa duniani vina umuhimu gani kwa watu?.Najua majibu ya ubongo wako hayatotofautiana sana na fikra zangu.Ila sentesi hii imekuwa haina mahusiano na  bara letu la Afrika ,hasa nchi yetu Tanzania.ukiwa mtanzania lazima utakataakataa kuunga mkono sentesi hii,Hasa pale uinapoona vitu vyenye thamani havisaminiwi wala kutiliwa maanani.

    Kuna watu wengi sana ni muhimu kwenye jamii yetu ila hawathaminiwi.pia vipo vingi vyenye thamani lakini tumevipuuzia.Moja ya watu muhimu tusiowathamini kwenye jamii yetu  ni walimu.Walimu wana hali ngumu sana hata wagosi wa kaya walishawai kuwaimbia.Ukiangalia watu wote wenye thamani wamepitia kwenye mikono ya mwalimu,Walimu wamekuwa kama makopo ya chumvi yainahifadhi chumvi na kufanya chumvi iwe salama mpaka wakati wa kuandaa chakula.Lakini ukichunguza makopo mengi ya chumvi mara nyingi hayawi kwenye hali ya usafi.Mpishi bila chumvi hawezi kupika chakula,lakini hasilani hawezi kukumbuka umuhimu wakifaa  kinachohifadhi chumvi hiyo.

     Huku kwenye soka pia  tunayo makopo yetu ya chumvi.Makopo hayo ni kama mengine kuhusu swala la kuthaminiwa.Makocha wengi sana Tanzania hawathaminiwi,Hivi juzi tu tumetoka kusikia malalamiko ya makocha wazawa.Hakuna anayewajali ,Ila lengo langu si kuwazungumzia wakina Julio,Msolla,Kayuni na wengine ambao angalau walishawai kupata nafasi ya kutoa walichonacho.Hapa nataka niwazungumzie makocha wenye uwezo mkubwa lakini hawathaminiwi kama makopo ya chumvi ya wapishi wengi.

    Wangapi wanamjua Hamisi chilemba?.Huyu jamaa blangata yake imesimama vilivyo kwenye soka.Hapa wachezaji kama uhuru selemani wataelewa ninachomaanisha.Uhuru selemani chumvi nzuri inayopika mabao Simba ila kopo lake Chilemba lipo kawe linashona viatu.Watu kama chilemba wana ujuzi mkubwa sana kwenye kukuza wachezaji chipukizi ila hawajawezeshwa na hakuna anayewathamini.Mtu kama chilemba sio wa kuwa mshona viatu.Angekua nchi za wenzetu chilemba angekua kwenye akademi ya soka akienendelea kukitumia kipaji chake maridhawa kuzlisha vipaji vya vijana chipukizi,Lakini kwetu Tanzania ataendelea kuwa mshona viatu huku wajanja wajanja wachache wasio na ujuzi bali vyeti vingi wakiendelea kutafuna fursa chache zilizopo.

     Hawa wakina chilemba wapo wengi sana nchini.Kuna watu kama Zagalo ni moja wa makocha waliowatoa wachezaji ligi kuu lakini hakuna anayetambua mchango wake.Kuna mzee wa makamo mmoja  anaitwa John Memba,wengi hupenda kumuita ‘coach memba’.Huyu mtu ana moyo wa dhati kujitolea kukuza soka la vijana,Mpaka sasa ‘coach memba’ ameshafanikiwa kutoa wachezaji 11 ambao wapo kwenye academi ya azam,wachezaji watano kwenye timu ya Ashanti na wachezaji  3 pan Afrika.Lakini mbaya zaidi amefanikiwa kutoa wachezaji watano kwenda kwenye akademi ya Qatar,Tusishangae wachezaji hao kuvaa uzi wa timu ya taifa ya Qatar wakiiwakilisha kwenye kombe la Dunia mwaka 2022.Huyu ndie John memba,sisi kwetu sio wa thamani ndio maana tumeamua kumtumia john memba kama mlinzi katika shule ya Benjamin mkapa,ila waqatar siku moja watarudi kumshukuru kwa mchango wake kwao.Wapo wengi wanaofanya hizi kazi kwa mapenzi yao ya dhati,Nakumbuka nilishawai kumuuliza kiongozi mmoja wa simba c ndugu akramu msangi al maarufu ‘aki mido’ ni jinsi gani ananufaika na timu hiyo akaniambia kuwa “nafanya kazi bila malipo yoyote”.Ni mapenzi ya namna gani haya.Huyu jamaa nae sifa yake kubwa ni kutafuta vipaji na kuvipeleka kwenyeakademi za  timu mbalimbali nchini  ikiwemo azam na mtibwa sugar.Simba hawajali wala kutambua mchango wake.Lakini Barcelona wanajua mchango wa Julio cosma aliyekua anafanya kazi kama za aki mido.Hata timu kubwa kumbe hazijali makocha wao wa chini?.

     Ukiangalia makocha hawa hawahitaji pesa bali wanahitaji kutoa walichonacho kichwani kwa maendeleo ya Soka letu.Hapa tff na vilabu vyetu  inabidi wawatengenezee makocha hawa miundombinu ya kufanya kazi walizoitiwa Duniani.Muda ambao chilemba anautumia kushona viatu angekua anautumia kwenye akademi ya soka angekuwa ameshazalisha wakina uhuru selemani zaidi ya watano mpaka sasa.Muda ambao mzee memba anautumia kulinda geti la shule ya Benjamin mkapa  angekua ameshagundua vipaji vya vijana zaidi ya hao aliyowagundua na kuwapeleka kwenye akademi mbali mbali za soka kupata mafunzo zaidi .Chonde chonde kwa vilabu msiendelee kuyaacha makopo haya yakiwa machafu jikoni,huku nyinyi mkiendelea kutumia chumvi walizozihifadhi kupikia chakula kitamu mnachokula sasa.Pia tff inabidi  mtafute njia ya kuyahifadhi makopo haya kwa kujenga na kuendeleza akademi za soka kwa maendeleo ya soka letu.

                                                                               
                                                                     

             
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOPO LA CHUMVI CHAFU JIKONI CHAKULA KITAMU TAYARI MEZANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top