728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, December 15, 2015

    FAROUK MIYA ATWAA UCHEZAJI BORA WA MWAKA UGANDA.

    Munyonyo,Uganda.

    Mshambuliaji aliye katika kiwango bora kwasasa nchini Uganda Farouk Miya juzi jumapili aliibuka kidedea baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa nchi hiyo. 
    Miya aliyeiongoza Uganda Cranes kutwaa kombe la Chalenji nchini Ethiopia mwezi huu ametwaa tuzo hiyo inayojulikana kama Airtel-Fufa Player of the Year baada ya kuwashinda Kezironi Kizito anayecheza nae katika klabu ya Vipers na nyota wa Orlando Pirates Yasser Mugerwa. 

    Mbali ya tuzo hiyo pia Miya amezawadiwa gari dogo aina ya Toyota Premio kama zawadi ya kuwa mchezaji bora wa mwaka.

    Nyota wengine waliotwaa tuzo mbalimbali ni:

    Mchezaji bora kwa upande wa wanawake: Sandra Nabweteme

    Tuzo ya Fufa Presidential : Paul Ssali

    Kocha bora wa mwaka: Faridah Bulega

    Mwamuzi bora wa mwaka: Mark Sonko

    Tuzo ya Fufa Fairplay: SC Villa

    Mpira wa ufukweni: Douglas Muganga

    Mchezaji kipenzi cha mashabiki Uganda: Tony Mawejje

    Mchezaji kipenzi cha mashabiki Afrika: Andre
    Ayew (Ghana & Swansea)


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: FAROUK MIYA ATWAA UCHEZAJI BORA WA MWAKA UGANDA. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top