728x90 AdSpace

Tuesday, December 15, 2015

FAROUK MIYA ATWAA UCHEZAJI BORA WA MWAKA UGANDA.

Munyonyo,Uganda.

Mshambuliaji aliye katika kiwango bora kwasasa nchini Uganda Farouk Miya juzi jumapili aliibuka kidedea baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mwaka wa nchi hiyo. 
Miya aliyeiongoza Uganda Cranes kutwaa kombe la Chalenji nchini Ethiopia mwezi huu ametwaa tuzo hiyo inayojulikana kama Airtel-Fufa Player of the Year baada ya kuwashinda Kezironi Kizito anayecheza nae katika klabu ya Vipers na nyota wa Orlando Pirates Yasser Mugerwa. 

Mbali ya tuzo hiyo pia Miya amezawadiwa gari dogo aina ya Toyota Premio kama zawadi ya kuwa mchezaji bora wa mwaka.

Nyota wengine waliotwaa tuzo mbalimbali ni:

Mchezaji bora kwa upande wa wanawake: Sandra Nabweteme

Tuzo ya Fufa Presidential : Paul Ssali

Kocha bora wa mwaka: Faridah Bulega

Mwamuzi bora wa mwaka: Mark Sonko

Tuzo ya Fufa Fairplay: SC Villa

Mpira wa ufukweni: Douglas Muganga

Mchezaji kipenzi cha mashabiki Uganda: Tony Mawejje

Mchezaji kipenzi cha mashabiki Afrika: Andre
Ayew (Ghana & Swansea)


  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: FAROUK MIYA ATWAA UCHEZAJI BORA WA MWAKA UGANDA. Rating: 5 Reviewed By: Unknown