728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, December 27, 2015

    DIEGO COSTA NJE MCHEZO WA JUMATATU DHIDI YA MANCHESTER UNITED

    London,England.

    Mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Muhispania Diego Costa anatarajia kuukosa mchezo wa siku ya jumatatu wa ligi kuu England utakaochezwa Old Trafford dhidi ya Manchester United baada ya kuwa na kadi tano za njano.

    Costa,26 ambaye jana jumamosi aliifungia Chelsea mabao mawili katika mchezo uliokwisha kwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Watford alilimwa kadi ya njano baada ya kuonyesha mchezo usio wa kiungwana na hivyo kufikisha kadi tano za njano ambazo humfanya mchezaji husika akose mchezo mmoja.

    Kutokana na kukosekana kwa Costa katika mchezo wa jumatatu Chelsea italazimika kuwatumia Radamel Falcao ama Loic Remmy katika safu yake ya ushambuliaji 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: DIEGO COSTA NJE MCHEZO WA JUMATATU DHIDI YA MANCHESTER UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top