728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, December 17, 2015

    AUBAMEYANG,MKHITARYAN WAIPELEKA BORUSSIA DORTMUND ROBO FAINAL DFB POKAL

    Dortmund, Ujerumani.

    Borussia Dortmund imetinga robo fainali ya michuano ya kombe la DFB Pokal baada ya kuitandika FC Augsburg kwa jumla ya mabao 2-0 katika mchezo wa hatua ya 16 uliopigwa katika dimba la Augsburg Arena jana usiku.

    Mabao yaliyopita ushindi Borussia Dortmund ambayo msimu uliopita ilipoteza mchezo wa fainali yamefungwa kipindi cha pili dakika za 61 na 72 na washambuliaji Emerick Aubameyang na Henrikh Mkhitaryan.

    Kufuatia ushindi huo Borussia Dortmund itavaana na VFB Stuttgart katika mchezo wa robo fainali utakaopigwa kati ya Februari 9 na 10 huku nusu fainali ikiwa April 19 na 20 na fainali ikichezwa Mei 21.

    Michezo ya robo fainali itakuwa kama ifuatavyo..

    VfB Stuttgart vs. Borussia Dortmund
    VfL Bochum vs. Bayern München
    Heidenheim vs. Hertha Berlin
    Bayer Leverkusen vs. Werder Bremen


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: AUBAMEYANG,MKHITARYAN WAIPELEKA BORUSSIA DORTMUND ROBO FAINAL DFB POKAL Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top