728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, December 14, 2015

    YANGA YAMBANA NIYONZIMA



    Haruna Niyonzima amekuwa akichelewa kurejea kikosini, hii imekuwa ni dharau ya muda mrefu kwa viongozi na wanachama wa Yanga. Sasa wamechoka!

    Yanga imecharuka kuhusiana na Haruna Niyonzima kuonyesha dharau kwa uongozi na wanachama wa klabu hiyo Goal imegundua.

    Katibu Mkuu wa Yanga, Dk Jonas Tiboroha alikaririwa na Saleh Jembe amesema wamekuwa hawafurahishwi kwa muda mrefu sasa kutokana na tabia za Niyonzima za kuchelewa kujiunga na kikosi kila anapokwenda Rwanda.

    “Niyonzima amekuwa na tabia ambayo si nzuri kwa maana ya nidhamu kila anapokuwa kwao Rwanda. Mfano tumemruhusu kwenda kuitumikia Rwanda katika michuano ya kimataifa, hadi sasa hajarejea.

    “Angalia mchezaji wa Azam FC kama Mugiraneza ambaye anacheza timu moja na Haruna amesharejea, wachezaji wa Simba waliocheza fainali wako katika klabu yao.

    “Niyonzima hajarejea na wala hasemi lolote. Si Jambo sahihi na hili linaonyesha tabia isiyo sahihi kwa maana ya kuheshimu majukumu yake katika klabu,” alisema Dk Tiboroha.

    “Haruna amekuwa akifanya hivi mara kwa mara, lakini sasa tumechoka na kama tutachukua hatua kali, basi wanachama wajue kabisa mapema.


    “Tumekuwa tukitoa adhabu kwake mara kadhaa, lakini mambo hayabadiliki. Wakati mwingine tumemkata mshahara hadi sasa tunaona kama tumechoka, lakini mambo ni yaleyale.”
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: YANGA YAMBANA NIYONZIMA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top