728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, March 19, 2017

    Liverpool yakaribia kumnasa Mesa


    Liverpool,England.

    MAJOGOO wa Merseyside,Liverpool wameripotiwa kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuinasa saini ya kiungo mshambuliaji wa Las Palmas ya Hispania, Roque Mesa Quevedo.

    Kwa mujibu wa taarifa  kutoka Ladbrokes News,ni kwamba msimu ujao Mesa,27, atakuwa mchezaji mpya wa Liverpool na kuhitimisha safari yake ya miaka mitano ya kuhudumu Gran Canaria.

    Jina la Mesa limekuja baada ya hivi karibuni kocha wa Liverpool,Jurgen Klopp kudaiwa kuwa yuko mawindoni akisaka kiungo mbunifu lakini atakayekuwa akipatikana kwa bei chee.

    Msimu huu Mesa amejizolea ujiko mkubwa Las Palmas baada ya kuichezea miamba hiyo michezo 24 na kuifungia bao moja huku akitoa pasi za mabao za kutosha.

    Dau la £15m limedaiwa kuwa litatosha kumnyakuwa Mesa ambaye pia anawindwa kwa ukaribu mkubwa na vilabu vya Tottenham na Everton.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Liverpool yakaribia kumnasa Mesa Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top