728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 20, 2016

    Ligi kuu bara:Vinara Simba SC dimbani tena leo,Jumamosi michezo sita kuchezwa


    Dar Es Salaam,Tanzania.

    LIGI KUU ya vodacom Tanzania Bara (VPL) itaendelea tena leo kwa mchezo mmoja kuchezwa katika dimba la uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam ambapo vinara wa ligi hiyo Wekundu wa Msimbazi,Simba SC,watakuwa wenyeji wa Mbao FC ya Mwanza.

    Simba SC wanaingia katika mchezo wa leo wakiwa kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa wamejikusanyia pointi 23 katika michezo tisa iliyopita.Ushindi katika mchezo wa leo utaendelea kuwaweka kileleni.

    Mbao FC wako nafasi ya kumi na moja baada ya kujikusanyia pointi 12 katika michezo kumi.Ushindi wowote leo utawafanya wafikishe pointi 15 na kuwapandisha mpaka nafasi ya sita.

    Ligi hiyo itaendelea tena Jumamosi Octoba 22 kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja mbalimbali ambapo mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa Kagera kuvaana na wenyeji wao Kagera Sugar.

    Jumamosi

    African Lyon v Mbeya FC

    Ndanda FC v Mwadui FC

    Mtibwa Sugar v Stand United

    Kagera Sugar v Yanga SC

    Majimaji FC v Ruvu Shooting

     Azam FC v JKT Ruvu 

    Jumapili

    Simba SC v Toto Africans

    Tanzania Prisons v Mbao FC

    Msimamo



    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Ligi kuu bara:Vinara Simba SC dimbani tena leo,Jumamosi michezo sita kuchezwa Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top