728x90 AdSpace

Thursday, October 20, 2016

Ligi kuu bara:Vinara Simba SC dimbani tena leo,Jumamosi michezo sita kuchezwa


Dar Es Salaam,Tanzania.

LIGI KUU ya vodacom Tanzania Bara (VPL) itaendelea tena leo kwa mchezo mmoja kuchezwa katika dimba la uwanja wa Uhuru jijini Dar Es Salaam ambapo vinara wa ligi hiyo Wekundu wa Msimbazi,Simba SC,watakuwa wenyeji wa Mbao FC ya Mwanza.

Simba SC wanaingia katika mchezo wa leo wakiwa kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa wamejikusanyia pointi 23 katika michezo tisa iliyopita.Ushindi katika mchezo wa leo utaendelea kuwaweka kileleni.

Mbao FC wako nafasi ya kumi na moja baada ya kujikusanyia pointi 12 katika michezo kumi.Ushindi wowote leo utawafanya wafikishe pointi 15 na kuwapandisha mpaka nafasi ya sita.

Ligi hiyo itaendelea tena Jumamosi Octoba 22 kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja mbalimbali ambapo mabingwa watetezi wa ligi hiyo Yanga watakuwa Kagera kuvaana na wenyeji wao Kagera Sugar.

Jumamosi

African Lyon v Mbeya FC

Ndanda FC v Mwadui FC

Mtibwa Sugar v Stand United

Kagera Sugar v Yanga SC

Majimaji FC v Ruvu Shooting

 Azam FC v JKT Ruvu 

Jumapili

Simba SC v Toto Africans

Tanzania Prisons v Mbao FC

Msimamo



  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: Ligi kuu bara:Vinara Simba SC dimbani tena leo,Jumamosi michezo sita kuchezwa Rating: 5 Reviewed By: Unknown