728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 19, 2016

    Ligi kuu bara:Michezo sita kuchezwa leo,mabingwa Yanga wako ugenini


    Dar Es Salaam,Tanzania.

    LIGI kuu ya Vodacom Tanzania Bara maarufu kama VPL itaendelea tena leo jioni kwa michezo sita kuchezwa kuchezwa katika viwanja sita vya miji mbalimbali nchini.

    Mabingwa watetezi wa ligi hiyo Young Africans watakuwa wageni wa Toto Africans huko CCM Kirumba,Mwanza huku matajiri wa jiji la Dar Es Salaam,Azam FC wao wakiwa nyumbani Chamazi Complex kuvaana na Mtibwa Sugar ya Manungu,Morogoro.

    Ndanda FC watakuwa nyumbani Nangwanda Sijaona kuwaalika vijana wa Mbeya City kutoka jijini Mbeya.Michezo mitano itachezwa saa 10:00 Jioni isipokuwa ule wa Azam FC wenyewe utachezwa saa 1:00 Usiku.

    Ratiba Kamili

    Toto Africans vs Young Africans

    Ndanda FC vs Mbeya City

    African Lyon vs Maji Maji

    Ruvu shooting vs Mwadui FC

    Tanzania Prisons vs Stand United

    Azam FC Vs Mtibwa Sugar FC (1:00) usiku


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Ligi kuu bara:Michezo sita kuchezwa leo,mabingwa Yanga wako ugenini Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top