728x90 AdSpace

  • Latest News

    Saturday, October 15, 2016

    Fainali klabu bingwa Afrika: Mamelodi Sundowns yaitwanga Zamalek tatu safiiiii


    Atteridgeville,Afrika Kusini.

    Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini imejiweka katika mazingira mazuri ya kutawazwa kuwa machampion wapya wa soka wa Afrika baada ya jioni ya leo kuifunga miamba ya Misri,Zamalek,kwa mabao 3-0 katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa fainali uliochezwa katika uwanja wa Lucas Moripe huko Atteridgeville,Afrika Kusini.

    Mabao yaliyoipa Mamelodi Sundowns ushindi katika mchezo wa leo yamefungwa na Anthony Laffor katika dakika ya 31, Tebogo Langerman katika dakika ya 40 na Percy Tau katika dakika ya 46.

    Sasa Mamelodi Sundowns inahitaji ushindi ama sare yoyote ile katika mchezo utakaochezwa wikendi ijayo huko Misri ili iweze kutwaa ubingwa huo ambao msimu uliopita ulitwaliwa na TP Mazembe ya Congo DR.

    Vikosi

    Mamelodi Sundowns: Onyango; Langerman,Nthethe, Arendse (Soumahoro 70'), Mbekile -Kekana (T. Zwane 85'), Mabunda - Dolly, Tau,Laffor - Billiat (Modise 65')

    Zamalek: Elshenawy (Elrehim 63'); Maroof,Eslam Gamal, Al Gabr, Tawfik - Ohawuchi,Ibrahim Salah, Tarek Hamed - Shikabala (Ramzi 55'), Hefny, Morsy (Mohamed Fathi 76')


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Fainali klabu bingwa Afrika: Mamelodi Sundowns yaitwanga Zamalek tatu safiiiii Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top