728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, October 12, 2016

    LIGI KUU BARA:YANGA 3,MTIBWA 1,SIMBA YAIDUNDA MBEYA CITY,AZAM FC HOI KWA STAND UNITED

    Dar Es Salaam,Tanzania.

    LIGI KUU ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) imeendelea tena leo Jumatano kwa michezo saba kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini.

    Yanga ikiwa katika uwanja wake wa nyumbani wa Uhuru imeichapa Mtibwa Sugar toka Manungu,Morogoro, kwa mabao 3-1.

    Mabao ya Yanga yamefungwa na Obrey Chirwa dakika ya 45,Simon Msuva dakika ya 68 na Donald Ngoma dakika ya 80 akimalizia kazi safi ya Geoffrey Mwashiuya. Bao la Mtibwa Sugar limefungwa na Haruna Chanongo dakika ya 63.

    Vinara wa ligi hiyo Simba wameichapa Mbeya City kwa jumla ya mabao 2-0 huko katika dimba la uwanja wa Sokoine Mbeya.

    Mabao ya Simba yamefungwa na Ibrahim Ajib kwa mpira wa adhabu pamoja na Shiza Kichuya kwa mkwaju mkali baada ya kuwazidi mbio mabeki wa Mbeya City.

    Stand United ikiwa katika uwanja wake wa nyumbani wa CCM Kambarage imeichapa Azam FC kwa bao 1-0 lililofungwa na Adam Salamba.

    Matokeo Mengine 

    Mbao FC 2 -0 Toto Africans
    Stand United 1-0 Azam FC
    Mwadui FC 2-0 African Lyon.
    Majimaji FC 0-1 Kagera Sugar
    JKT Ruvu 0-0 Tanzania Prisons

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: LIGI KUU BARA:YANGA 3,MTIBWA 1,SIMBA YAIDUNDA MBEYA CITY,AZAM FC HOI KWA STAND UNITED Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top