728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 14, 2016

    Unamtaka Gareth Bale basi andaa Euro Milioni 500

    Madrid,Hispania.

    HATARI!!Real Madrid imenogewa na huduma za staa wake kutoka Wales,Gareth Bale na katika kuonyesha kuwa imekufa kwa mkali huyo anayejua vyema kuutumia mguu wake wa kushoto tayari imemuandalia mkataba mpya na mnono wa miaka sita.

    Kwa mujibu wa taarifa kutoka katika kituo cha Radio Cadena Ser cha Hispania,mkataba huo mpya utamfanya Bale,27,aendelee kubaki Santiago Bernabeu mpaka mwishoni mwa msimu wa 2021-22.

    Aidha katika mkataba huo mpya Real Madrid imeweka kipengele cha kumuuza mkali huyo wa zamani wa Tottenham kwa ada ya uhamisho ya Euro Milioni 500 (Paundi 427)


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Unamtaka Gareth Bale basi andaa Euro Milioni 500 Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top