728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, October 27, 2016

    Robo fainali EFL:Arsenal v Soton,Man United v Westham,Droo kamili iko hapa


    London,England.

    DROO ya michuano ya kombe la ligi maarufu kama EFL imefanyika jana Jumatano Usiku muda mfupi baada ya kumalizika kwa michezo ya hatua ya 16 bora.

    Manchester United ambayo imetinga robo fainali kwa kuwabanjua wapinzani wao Manchester City kwa bao 1-0 itakutana na Westham United ambayo imeingia hatua hiyo kwa kuifunga Chelsea kwa mabao 2-1.

    Arsenal itakuwa Nyumbani Emirates kuvaana na Southampton wakati Leeds United wakisafiri mpaka Anfield kupepetana na Liverpool.Hull City watakuwa nyumbani KC Stadium kucheza na Newcastle United.

    Droo Kamili

    Liverpool v Leeds United

    Manchester United v West Ham United

    Hull City v Newcastle United

    Arsenal v Southampton

    Michezo yote ya robo fainali itachezwa kati ya Novemba 28/29


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Robo fainali EFL:Arsenal v Soton,Man United v Westham,Droo kamili iko hapa Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top