728x90 AdSpace

Thursday, October 27, 2016

Robo fainali EFL:Arsenal v Soton,Man United v Westham,Droo kamili iko hapa


London,England.

DROO ya michuano ya kombe la ligi maarufu kama EFL imefanyika jana Jumatano Usiku muda mfupi baada ya kumalizika kwa michezo ya hatua ya 16 bora.

Manchester United ambayo imetinga robo fainali kwa kuwabanjua wapinzani wao Manchester City kwa bao 1-0 itakutana na Westham United ambayo imeingia hatua hiyo kwa kuifunga Chelsea kwa mabao 2-1.

Arsenal itakuwa Nyumbani Emirates kuvaana na Southampton wakati Leeds United wakisafiri mpaka Anfield kupepetana na Liverpool.Hull City watakuwa nyumbani KC Stadium kucheza na Newcastle United.

Droo Kamili

Liverpool v Leeds United

Manchester United v West Ham United

Hull City v Newcastle United

Arsenal v Southampton

Michezo yote ya robo fainali itachezwa kati ya Novemba 28/29


  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: Robo fainali EFL:Arsenal v Soton,Man United v Westham,Droo kamili iko hapa Rating: 5 Reviewed By: Unknown