728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, October 07, 2016

    KOMBE LA DUNIA 2018:ARGENTINA YABANWA MBAVU YALAZIMISHA SARE YA 2-2 NA PERU

    Limma,Peru.

    ARGENTINA ikiwa ugenini Lima imeshindwa kutamba baada ya asubuhi hii kulazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na wenyeji Peru katika mchezo mkali wa kuwania tiketi ya kushiriki michuano ya kombe la dunia la mwaka 2018 huko nchini Urusi.

    Ramiro Funes Mori alianza kuiandikia Argentina bao la kuongoza dakika ya 15 ya mchezo kutokana na mpira wa kona wa Paul Dybala.Bao hilo lilidumu mpaka mapumziko.

    Kipindi cha pili wenyeji Peru walikuja juu na kufanikiwa kusawazisha bao dakika ya 58 kupitia kwa nahodha wao Paolo Guerrero.Bao hilo halikudumu sana kwani mnamo dakika ya 77 ya mchezo Gonzalo Higuaín aliifungia Argentina bao la pili. 



    Mchezo ukiwa unaelekea ukingoni madhambi ya mlinzi Ramiro Funes Mori yaliyofanywa kwa Paolo Guerrero yaliizawadia Peru penati iliyofungwa kwa ustadi mkubwa na Christian Cueva katika dakika ya 84' na kufanya mchezo uishe kwa sare ya mabao 2-2.

    Matokeo Mengine

    Ecuador 3 - 0 Chile

    Uruguay 3 - 0 Venezuela

    Paraguay 0 - 1 Colombia

    Brazil 5 - 0 Bolivia

    Peru 2 - 2 Argentina


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: KOMBE LA DUNIA 2018:ARGENTINA YABANWA MBAVU YALAZIMISHA SARE YA 2-2 NA PERU Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top