728x90 AdSpace

Monday, March 27, 2017

Mchezo wa Mbao FC na Simba SC wasogezwa mbele



Paul Manjale

MCHEZO wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL) kati ya wenyeji Mbao FC na Simba SC uliokuwa uchezwe Aprili 8, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza umesogezwa mbele kwa siku mbili zaidi na sasa utachezwa Aprili, 10.

                    
Taarifa iliyotolewa jioni ya leo na Mkurugenzi wa Bodi ya Ligi, Boniphace Wambura imesema mchezo huo umesogezwa mbele ili kupisha shughuli za kijamii zitakazofanyika kwenye uwanja huo kuanzia Aprili 1 mpaka Aprili 9.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: Mchezo wa Mbao FC na Simba SC wasogezwa mbele Rating: 5 Reviewed By: Unknown