728x90 AdSpace

Sunday, March 26, 2017

Msoma achaguliwa kuwa Mkurugenzi mpya wa ufundi Zanzibar



Lameck Francis.
(Unguja,Zanzibar)

Katika kuhakikisha Zanzibar inakuwa na mikakati thabiti kuhakikisha mpira unachezwa tofauti na mwanzo ambapo Zanzibar haikuwa na uwanachama katika shirikisho la mpira barani afrika,CAF ,Kamati Tendaji ya Chama cha Soka Visiwani Zanzibar “ZFA” leo imemchagua  rasmi kocha Abdulghany Msoma kuwa Mkurugenzi wa Ufundi “Technical Director” katika kikao ambacho kimefanyika kwenye Ukumbi wa Magereza uliopo Kilimani Mjini Unguja.

Akizungumza mara baada ya kumalizika mkutano huo Afisa habari wa ZFA Ali Bakari “Cheupe” amesema kamati tendaji ya ZFA wamemchagua Msoma kuwa Mkurugenzi wa Ufundi baada ya kuona kuwa anastahili nafsi hiyo hivyo anaweza kuitendea haki kwa kipindi hiki ambacho ligi kuu ya Zanzibar inatakiwa kubadilika kwa kufuata katiba mpya walipewa na Caf



Msoma baada ya kupatiwa nafasi hiyo amefurahishwa sana lakini kahimiza ushirikiano kati ya ZFA na wadau wengine ili kuinua soka la Zanzibar kwani linahitaji nguvu kubwa ili ligi iwe na mvuto na ushindani mkubwa kama zilivyo ligi nyingine.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: Msoma achaguliwa kuwa Mkurugenzi mpya wa ufundi Zanzibar Rating: 5 Reviewed By: Unknown