728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, March 30, 2017

    Chama cha soka Iringa chakiri mambo si shwari kati yake na Lipuli FC



    James Eduma,Iringa.

    Uongozi wa chama cha soka mkoani Iringa (IRFA) umekiri kutokuwepo kwa mahusiano mazuri  kati yao na viongozi wa klabu ya Lupuli FC ambao wana jukumu la kuiwezesha timu yao kujiandaa vyema kabla ya kuanza kwa ligi kuu ya soka Tanzania bara msimu wa 2017/18.

    Katibu mkuu wa IRFA, Ally Ngallah ameelezea sintofahamu hiyo iliyogubika miongoni mwa viongozi wa klabu hiyo kongwe hapa nchini, hadi kufikia hatua ya kutokua na uhusiano mzuri na chama cha soka mkoa wa Iringa.

    Hata hivyo Ngallah amesema uongozi wa IRFA unaendelea kupambana ili kumaliza sintofahamu ya viongozi wa Lupuli FC ili kusaidia mchakato wa kupatikana kwa mwenendo mzuri ambao utaisaidia klabu hiyo kufanya usajili wa wachezaji vizuri pamoja na kuwa na maandalizi mazuri ya ligi kuu.

    Katika hatua nyingine Ngallah amezungumzia uwanja wa Samora ambao utatumiwa na klabu ya Lipuli FC katika michezo ya ligi kuu msimau ujao wa ligi, kwa kusema upo katika hali nzuri na umekidhi vigezo.

    Amesema uwanja huo umefanyiwa marekebisho ya hali juu baada ya kupokea taarifa za maelekezo kutoka TFF.







    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Chama cha soka Iringa chakiri mambo si shwari kati yake na Lipuli FC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top