728x90 AdSpace

  • Latest News

    Tuesday, March 28, 2017

    TFF yapokea kwa masikitiko kifo cha Mkurugenzi wake wa fedha wa zamani



    Dar Es Salaam,Tanzania.

    Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi wake wa Fedha na Utawala, marehemu Edgar Masoud.

                                              

    Edgar Masoud aliyefariki dunia jana jioni Machi 27, 2017 aliugua ghafla juzi Jumapili akiwa kanisani kabla ya kukimbizwa Hospitali ya Bochi iliyoko Mbezi kwa Msuguri ambako alikutwa na mauti akipatiwa matibabu.

    Kwa mujibu wa familia, Mwili wa marehemu Edgar Masoud unatarajiwa kupumzishwa kesho Jumatano Machi 29, mwaka huu kwenye makaburi ya Mkuranga mkoani Pwani.



    Familia imetoa taarifa kuwa taratibu za mazishi zinafanyika nyumbani kwake Kimara Kibo jijini Dar es Salaam.



    Kwa nafasi ya pekee, katika salamu zake za rambirambi, Rais wa TFF, Jamal Malinzi alitoa wito kwa ndugu, jamaa, majirani na marafiki kuwa watulivu katika kipindi hiki kigumu kwa wanafamilia nzima ambao wampoteza mpendwa wao
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TFF yapokea kwa masikitiko kifo cha Mkurugenzi wake wa fedha wa zamani Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top