728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, March 29, 2017

    TFF yaikosoa Yanga SC



    James Eduma,Iringa.

    Shirikisho la soka nchini TFF limekosoa mpango wa mabingwa wa soka Tanzania bara Young Africans wa kutaka kuhamisha mchezo wao wa hatua ya mchujo wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya MC Alger ya Algeria kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

    Afisa habari wa TFF Alfred Lucas amesema mpango huo wa Young Africans hautowezekana kufuatia uwanja wa CCM Kirumba kutoka CAF ambao ndio wasimamizi wakuu wa michuano ya klabu bingwa Afrika pamoja na kombe la shirikisho.

    Alfred amesema mchezo wa Young Africans bado utaendelea kuchezwa jijini Dar es salaam katika uwanja wa Taifa, na kama uongozi wa klabu hiyo utaendelea na mpango wa kuhamisha mchezo wao dhidi ya MC Alger, wana nafasi ya kuupeleka Azam Complex ama Aman Zanzibar.

    Wakati huo huo shirikisho la soka nchini TFF limekanusha taarifa za kupangwa kwa tarehe ya mchezo wa hatua ya robo fainali kati ya Young Africans dhidi ya Tanzania Prisons wa kombe la shirikisho.
    Alfred Lucas amesema taarifa ziliozosambazwa katika mitandao ya kijamii kuhusu kupangwa kwa tarehe ya mchezo sio za kweli.

    Taarifa iliyosambazwa katika mitandao ya kijamii inaeleza kuwa mchezo wa Young Africans na Tanzania Prisons wa kombe la shirikisho umepangwa kuchezwa Aprili 22.





    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: TFF yaikosoa Yanga SC Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top