728x90 AdSpace

  • Latest News

    Sunday, March 26, 2017

    Ligi kuu Zanzibar sasa kushirikisha vilabu 12 pekee,ligi daraja la pili kuvunjwa



    Francis Lameck
    Unguja

    Ligi kuu soka ya Zanzibar msimu wa mwaka 2017-2018 itashirikisha vilabu 12 pekee kwa Zanzibar nzima na itakuwa ikichezwa kwa kanda mbili tofauti kwa kanda ya Pemba na kanda ya Unguja.

    Kwa mujibu wa Makamu wa Urais wa ZFA Pemba, Ali Mohammed amesema baada ya kupatiwa uanachama wa kudumu kutoka Shirikisho la soka Barani Afrika wametakiwa kupunguza timu na kubakiwa na timu 12 tu kwa msimu ujao.

    Wadau wengi wa soka Visiwani Zanzibar wanahamu ya kujua vipi vilabu hivyo 12 vitapatikana ambapo jukumu hilo kwasasa wamepewa umoja wa vilabu kwa kukaa pamoja na vilabu vyao kwa kujadili mfumo gani watumie ili zipatikane timu hizo 12 kisha kuwarejeshea tena kamati tendaji ya ZFA kama walivyokubaliana.

    Aidha  kamati tendaji wataangalia mfumo ambao wameletewa na umoja wa vilabu kama watakuwa na uwezo wa kutoa ufafanuzi wataelezea na endapo kamati tendaji wakishindwa, litaenda kuamuliwa na kutolewa ufafanuzi katika mkutano mkuu ambao unatarajiwa kufanyika April 8 na 9, 2017 huko Kisiwani Pemba.

    Kwa upande wa ligi daraja la kwanza vilabu vitakavyoshuka msimu huu pamoja na vile ambavyo vitakavyobakia katika daraja hilo vitashiriki hata kama vitafika zaidi ya 30 wakati huo huo daraja la Pili Taifa linatarajiwa kuvunjwa.
                                                                    
    Pia msemaji wa  Zfa taifa amezungumzia namna ya upatikanaji wa pasposti za wachezaji wa Zanzibar ambao wataitumikia timu ya taifa ya Zanzibar nakusema wachezaji watakaotumika kwenye timu ya taifa ya Zanzibar ni wale wenye paspoti ya Mzanzibar. 


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Ligi kuu Zanzibar sasa kushirikisha vilabu 12 pekee,ligi daraja la pili kuvunjwa Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top