728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, March 29, 2017

    Haji Manara afichua kilichosababisha kufungiwa kwa Jerry Murro


    James Eduma,Iringa
    Mkuu wa idara ya habari na mawasilino wa klabu ya Simba Haji Manara, kwa mara ya kwanza amefichua siri ya kilichosababisha kufungiwa kwa aliyekua msemaji wa klabu ya Young Africans Jerry Muro.
    Manara amesema alichangia kufungiwa kwa Jerry Muro kwa kutumia udhaifu wa shirikisho la soka nchini TFF, ambalo kwa asilimia kubwa lilionekana kumfumbia macho Jerry Muro pale alipoonyesha kukosea kwa kutoa lugha ambazo hazikua za kiungwana katika michezo.
    Manara amesema alifanya mchezo huo kwa kutumia elimu aliyowahi kuipata nchini China.
    Hata hivyo Haji Manara amekiri kumiss Jerry Muro katika shughuli za usemaji wa klabu za Simba na Young Africans japo akaendelea kusisitiza rafiki yake alikosea kusimamia misingi ya mchezo wa soka ambayo inakataza maneno ya kashfa na kejeli.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Haji Manara afichua kilichosababisha kufungiwa kwa Jerry Murro Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top