728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, September 23, 2015

    WENGER ABWAGANA NA MKE WAKE,AMGEUKA GIROUD ASEMA SIYO CHAGUO NAMBA MOJA TENA


    London,England.

    Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ameachana na mke wake Annie baada ya miaka mitano ya ndoa.

    Wawili hao wameachana baada ya uvumi wa miezi kadhaa kuwa uhusiano wao uko hobelahobela huku sababu kubwa ikiwa na kukosekana kwa maelewano ndani ya nyumba kuliko sababishwa na Wenger kuwa bize sana na kazi ya ukocha.

    Wenger na Annie, 59, walifunga ndoa mwaka 2010 baada ya kuwa wachumba kwa kipindi kirefu.Mpaka wanaachana tayari wamefanikiwa kuwa na binti mmoja aitwaye Leah,18.Taarifa zaidi zinadai wawili hawajawahi kupiga picha ya pamoja tangu mwaka 2013. 

    Wakati huohuo Arsene Wenger amemwambia mshambuliaji Olivier Giroud kuwa siyo chaguo namba moja tena klabuni hapo na badala yake anapaswa kugombania namba na Theo Walcott katika safu ya ushambuliaji na atarajie kuanzia benchi katika mchezo wa leo wa Capital One dhidi ya Tottenham.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WENGER ABWAGANA NA MKE WAKE,AMGEUKA GIROUD ASEMA SIYO CHAGUO NAMBA MOJA TENA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top