728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, September 16, 2015

    VPL:SIMBA WAPANGA KUIFANYIA KITU MBAYA MGAMBO LEO MKWAKWANI

    KAMA kuna kitu ambacho Simba inatakiwa kukifanya leo Jumatano ili kuwafurahisha wanachama, wapenzi na mashabiki wake ni kupata ushindi dhidi ya Mgambo JKT katika mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambapo wachezaji wa timu hiyo wameapa kwamba wapinzani wao hao ni 'lazima wakae.'

    Simba haijawahi kuifunga Mgambo kwenye Uwanja wa Mkwakwani tangu timu hiyo inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa ilipopanda daraja na zaidi Wekundu hao wamekwishaambulia sare moja na kufungwa mechi mbili.

    Katika kuhakikisha wanaibuka na ushindi katika mchezo huo, Kocha wa Simba, Mwingereza Dylan Kerr, ameonekana kutaka wachezaji wake kupiga pasi 100 bila kupoteza kwa adui.
    Katika mazoezi yao yaliyofanyika juzi asubuhi kwenye Uwanja wa Disuza, Kerr alitumia muda mwingi kutaka wachezaji wake kupiga pasi nyingi zinazofika ili waweze kuibuka na ushindi.

    (Kwa habari kamili usikose kujipatia nakala yako ya Gazeti la DIMBA Leo)

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: VPL:SIMBA WAPANGA KUIFANYIA KITU MBAYA MGAMBO LEO MKWAKWANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top