728x90 AdSpace

Thursday, September 17, 2015

MAN UNITED YAJA JUU BAADA YA UEFA KUTOA TUZO KWA ALIYEMVUNJA LUKE SHAW


Manchester,England.

Unaweza kusema vyovyote vile unavyojisikia lakini maamuzi ya shirikisho la vilabu vya soka barani Ulaya (UEFA) hayawezi kubadilika.

Taarifa kutoka England zinasema klabu ya Manchester United imelijia juu  shirikisho la vilabu vya soka barani Ulaya UEFA kwa kitendo chake cha kumpa tuzo mchezaji ya mchezaji bora wa mechi mlinzi wa PSV Endhoven Hector Moreno ambaye alimchezea rafu na kumvunja mara mbili mlinzi wake wa kushoto Luke Shaw katika mchezo wa kwanza wa ligi ya mabingwa jumanne iliyopita.
Luke Shaw reacts after sustaining an injury
Manchester United imeponda vikali uteuzi huwa kwa madai kuwa mtu aliyefanya unyama kwa mwinzie kiasi kile hakupaswa kupewa tuzo yenye heshima kama ile.

Moreno alimrukia na kumvunja mifupa miwili ya mguu wa kulia Luke Shaw dakika ya 16 ya mchezo huo ulioisha kwa Manchester United kulala kwa goli 2-1.Luke Shaw atakuwa nje ya uwanja kwa kipindi cha miezi sita akiuguza jeraha hilo
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: MAN UNITED YAJA JUU BAADA YA UEFA KUTOA TUZO KWA ALIYEMVUNJA LUKE SHAW Rating: 5 Reviewed By: Unknown