728x90 AdSpace

Wednesday, September 30, 2015

UBABE UBABE TU:MWAMUZI APIGWA TEKE,KOFI AJIBU KWA KUTOA BUNDUKI UWANJANI

BURUDANI.Mwamuzi mmoja wa soka nchini Brazil ameingia matatani baada ya kuonyesha kitako cha bunduki aina ya bastola kama ishara ya kujilinda dhidi ya wachezaji waliokuwa wakimshushia kipigo uwanjani kufuatia kutoridhishwa na maamuzi yake.

Mwamuzi huyo Gabriel Murta ambaye pia ni ofisa wa polisi alilazimika kuikumbuka bastola yake iliyokuwa kiunoni baada ya kupigwa teke kisha ngumi na wachezaji wa klabu ya Belo wakati akichezesha mechi ya soka ya daraja la chini nje kidogo ya jiji la Belo Horizonte.

Wakati huo huo mwenyekiti wa chama cha soka cha eneo hilo Giuliano Bozzano amesema Mutra atatafutiwa mwanasaikolojia ili amuweke sawa kiakili baada ya tukio hilo.



  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: UBABE UBABE TU:MWAMUZI APIGWA TEKE,KOFI AJIBU KWA KUTOA BUNDUKI UWANJANI Rating: 5 Reviewed By: Unknown