728x90 AdSpace

  • Latest News

      Monday, September 28, 2015

      BAADA YA NYOSO KUMDHALILISHA BOCCO,MALINZI AJA JUU


      September 27 katika mechi kati ya Azam FC dhidi ya Mbeya City mchezo uliochezwa katika uwanja wa Azam Complex Mbande Chamazi, nahodha wa Mbeya City Juma Nyoso alimfanyia kitendo cha kidhalilishaji nahodha  wa Azam FC John Bocco, licha ya kuwa muamuzi hakuona ila kupitia picha za mnato na kanda za video tukio hilo lilinaswa na kusambaa katika mitandao ya kijamii.

      Rais wa Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF Jamal Malinzi amethibitisha hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mchezaji aliyefanya kitendo hicho, Malinzi amethibitisha hilo kupitia account yake rasmi ya twitter. Lakini hii sio mara ya kwanza kwa beki na nahodha wa Mbeya City Juma Nyoso kufanya kitendo hicho, alishawahi kumfanyia Elias Maguli na kupewa adhabu ya kufungiwa mechi nane mwanzo mwa mwaka 2015.
      • Blogger Comments
      • Facebook Comments

      0 comments:

      Post a Comment

      Item Reviewed: BAADA YA NYOSO KUMDHALILISHA BOCCO,MALINZI AJA JUU Rating: 5 Reviewed By: Unknown