728x90 AdSpace

  • Latest News

    Wednesday, September 23, 2015

    BAADA YA FERGUSON KUDAI ANAMCHUKIA,WAKALA WA POGBA AJIBU MAPIGO ADAI FERGUSON HAJUA ANACHOKIONGEA


    Mino Raiola ambaye ni wakala wa kiungo wa Juventus Paul Pogba ameibuka na kumpinga kocha wa zamani wa Manchester United Alex Ferguson aliyedai kuwa hampendi Raiola kwakuwa alishawishi Pogba kuondoka Manchester United mwaka 2012.

    Raiola amejibu mapigo hayo baada ya Ferguson kuandika katika kitabu chake kiitwacho Leading kuwa kuna mawakala wawili anaowachukia huku mmoja wao akiwa ni Mino Raiola.Raiola alimshawishi pogba agomee mkataba mpya wa kubaki Manchester United na badala yake aende zake Juventus.Raiola pate pesa za bure kwani Pogba alikuwa amemaliza mkataba wake.
    Raiola amesema "Feguson hajui anachokiongea.Maneno hayo hayaiathiri kazi yangu katika njia hasi bali ni kama uthibitisho kuwa naijua kazi yangu vizuri.Leo Pogba ana thamani inayokaribia paundi milioni 100.

    "Nilifanya kile nilichoona kuwa ni chenye faida kwa mchezaji wangu,ningetaka faida yangu mwenyewe basi ningeacha Pogba abaki Manchester United.Nilichokifanya ni kuweka maslahi ya Pogba mbele tukafikia maamuzi na kukahamia Turin.Labda Ferguson anawapenda watu wanaomtii.Kutoka katika nukuu yake,nadhani Ferguson bado hafahamu kuwa Pogba ni nani.

    'Ferguson doesn't have a clue' - Raiola hits back at Pogba criticism
    "Ferguson alikuwa ni kocha mzuri lakini pia makocha wazuri nao kuna wakati wanakosea mambo"
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: BAADA YA FERGUSON KUDAI ANAMCHUKIA,WAKALA WA POGBA AJIBU MAPIGO ADAI FERGUSON HAJUA ANACHOKIONGEA Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top